Instagram story viewer> @dktabbasi> Post
6 days ago
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of airplane and text that says 'Ταηζαία'.
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of one or more people, aircraft and text.
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of airplane and text.
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of airplane and text.
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of airplane and text.
Photo by Hassan Abbas on July 20, 2026. May be an image of one or more people, bus and text.
32
Posted On: July 20th 2026, 04:50 pm
Ulikuwa wakati wenye tafakuri nyingi leo Jumatatu, Julai 20, 2026, jijini Dar es Salaam nilipotembelea Makumbusho ya Taifa na kujionea usimikaji wa Ndege yetu aina ya Fokker F28-3000 (Charlie Charlie Mike), ndege ambayo ilitumiwa na marais wetu kuanzia mwaka 1978 ikiwa ni Awamu ya kwanza ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, mpaka mwaka 2018 katika Awamu ya Tano ya utawala wa nchi yetu chini ya Dkt. John Pombe Magufuli ilipohamishiwa katika majukumu mengine.

Ndege hii ambayo unaweza kuitembelea pale Makaumbusho ya Taifa, Dar es Salaam, sasa imehifadhiwa ili kuenzi mchango wake usiomithilika katika ukombozi wa Bara la Afrika, alama ya miaka 40 ya utekelezaji wa diplomasia yetu ya nchi ikisafiri kote duniani lakini ikiwa ni ushahidi na mwanga wa matumaini uliowaangazia viongozi wetu kila kona ya nchi hii na kufika mikoani katika kutekeleza majukumu yao ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Fokker 28 ni alama ya sisi ni nani, tumetoka wapi, tunakwenda wapi; na ni alama ya Afrika, Tanzania na uongozi wetu. Karibu uone alipokuwa anakaa Mwalimu Nyerere, kiti cha maamuzi alichomrithisha Mzee Mwinyi Mkapa, Mzee Kikwete na baadaye Mzee Magufuli na namna viongozi wetu walivyofanya maamuzi mengi juu ya ndege hii ya matumaini.

Fokker 28 5H Ni urithi wetu! Ni Sisi!
Comments (32)
ndalakasheba1 4 days ago

ndalakasheba1

🔥🔥🔥🔥👏👏👏👏

darlingtondavis_ 4 days ago

darlingtondavis_

Charlie charlie mike 👏👏

mchomachiki 5 days ago

mchomachiki

Tunasonga mbele 🔥🔥🔥

muroalbert62 5 days ago

muroalbert62

na Ile ndege ya Mzee Mkapa ambayo Basili Mramba alituambia Bora tule Nyasi ipo wap nayo inaistoria nying sana

kumbo_waterwelldrilling 5 days ago

kumbo_waterwelldrilling

HUDUMA ZA VISIMA NA MIFUMO YA MAJI 🌊 Kwa mahitaji ya: ✔️ Geo Physical / Hydro Geological Survey ✔️ Uchimbaji wa Kisima (Borehole Drilling) ✔️ Kusafisha Kisima (Borehole Flushing) ✔️ Ukarabati wa Kisima (Borehole Rehabilitation) ✔️ Ufungaji wa Pump (Pump Installation) ✔️ Upimaji wa Wingi wa Maji (Pumping Test) ✔️ Ufungaji wa Bomba (Plumbing Installation and Services) ✔️ Jambo lolote linalohusiana na kisima usisite kuwasiliana nasi 💯 Sisi ni moja kati ya suluhisho bora ya kisima chako na mifumo ya maji 🏡 Ni kwa aina zote za visima vifupi na virefu, na kwa matumizi ya aina zote iwe: Shamba • Nyumbani • Kiwandani • Shule • Mgodini n.k 📞 NB: USHAURI NI BURE Wasiliana nasi: 0653166048

octamshiu 5 days ago

octamshiu

Kwa mwaka huo 1978 itakuwa ilikua one of the best duniani .. ikumbukwe pia kuwa kabla ya mwaka 1978 kuingia vitani ndio wakati Export za Tanzania zilikua juu ya Imports … ( favorable balance of trade / payments ) … tukiuza sana Mkonge ; Pamba ; Kahawa etc kabla ya Hali ya uchumi wa dunia pia kutuvuruga .. we have to be proud of our country and history

stert6116 5 days ago

stert6116

Wazo zuri. Shida ukiambiwa gharama za kufanikisha zoezi hilo ndio utajua hujui !

1worldsafaris_sports 5 days ago
dickson_nghily 5 days ago

dickson_nghily

Hii ndege nimeipanda kipindi cha Rais Mkapa mwaka 2000, though wakati naipanda, safari hiyo ilikuwa ya Makamu wa Rais wa wakati huo, Hayati Dr Omar Ali Juma. Ninakumbuka kiti nilichokaa coz nilikuwa namtizama Makamu wa Rais, na ilikuwa safari yangu ya kwanza kwa ndege, tena ndege ya rais. NITAITEMBELEA.

supersly90 5 days ago

supersly90

Hii nzuri sana.

bobo_vijora_pambe 5 days ago

bobo_vijora_pambe

Habari kuiona inagharimu kiasi?

mr_kilale 5 days ago

mr_kilale

👏👏👏👏👏

princemagari20 5 days ago

princemagari20

Aiseee lazima nikaitembeleee

ben_mwanantala_mzalendo 5 days ago
levano_tz 5 days ago

levano_tz

Saf sana

Load More

More posts

back to up