Instagram story viewer> @azamtvtz> Post
10 hours ago
5
Posted On: July 25th 2026, 04:41 pm
Majeruhi wa ajali mbalimbali jijini Mwanza waliolazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando kwa matibabu, wameiomba serikali kufunga kamera za ulinzi (CCTV) kwenye baadhi ya maeneo muhimu ya barabara, vikiwepo vivuko vya watembea kwa miguu ili iwe rahisi kubaini vyanzo vya ajali na kuharakisha uchunguzi.

Wakizungumza wakati wakipokea misaada ya kiutu kutoka kwa askari wa Jeshi la Polisi mkoani humo, wagonjwa hao wamemuambia Kamanda wa Polisi, DCP Wilbroad Mutafungwa kuwa, waathirika wengi wa ajali za barabarani hupoteza haki zao kutokana na kukosekana kwa ushahidi, huku wanaosababisha ajali hizo wakikwepa mkono wa sheria.

✍Innocent Aloyce
Mhariri | @abuuyusuftz

#AzamTVUpdates
Comments (5)
enock.vuhahulla.52 2 hours ago

enock.vuhahulla.52

Msisahau miundo mbinu pia

kibacha_md 10 hours ago

kibacha_md

Siku hizi barabarani ni utumbo mtupu. Hakuna cha taa wala zebra.

jozee_silvan 10 hours ago

jozee_silvan

@jozee_silvan👏👏👏👏👏

mr_t_mkopeshaji_simu 10 hours ago

mr_t_mkopeshaji_simu

🔥🔥🔥🔥🔥

More posts

back to up