Posted On: July 20th 2026, 07:20 pm
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Dalmia Mikaya, amefika katika eneo la Mtaa wa Majengo, Kata ya Vijibweni, kufuatilia mgogoro wa muda mrefu wa ardhi ulioibuka kufuatia malalamiko ya wananchi waliokuwa na hofu ya kubomolewa nyumba zao.
Akizungumza na wananchi, amesema ataunda kamati maalum itakayofuatilia chanzo cha mgogoro huo, kubaini changamoto zilizopo na kupendekeza suluhisho sahihi litakalomaliza mgogoro huo.
Host:
@godmuya