Posted On: July 25th 2026, 07:52 am
#HABARI Muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia umetangaza kumaliza operesheni yake dhidi ya Wahouthi wa Yemen baada ya kushambulia maeneo ya kijeshi ya kundi hilo kufuatia mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu.
Msemaji wa muungano huo, Turki al Maliki, amesema Wahouthi walilenga meli za kibiashara na kusababisha muungano kutoa “jibu kali na la kuamua” dhidi ya maeneo yanayotumiwa na kundi hilo.
Kwa mujibu wa chanzo cha usalama kilichonukuliwa na AFP, mashambulizi hayo yalilenga kambi na ngome za kijeshi za Wahouthi katika mkoa wa Hodeidah.
Runinga ya Al Masirah inayomilikiwa na Wahouthi imeripoti milipuko katika maeneo kadhaa, huku wakazi wakithibitisha kusikia mashambulizi makubwa.
Wahouthi wametishia kulipiza kisasi dhidi ya Saudi Arabia, wakidai mashambulizi hayo yalilenga miundombinu ya kiraia, huku wakisisitiza kuendelea kulenga maslahi ya Saudi baharini.
#EastAfricaTv #TogetherTunawakilisha