Posted On: July 25th 2026, 09:22 am
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa leo Julai 25, 2026 katika Uwanja wa Mnara wa Mashujaa, Dodoma.
Mbali ya Rais Samia, Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi ni miongoni mwa Viongozi waliokuwepo.
Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Julai 25 kwa lengo la kuwaenzi mashujaa waliopoteza maisha wakitetea, wakipigania na kulinda uhuru, amani na maslahi ya Taifa la Tanzania.
Katika maadhimisho hayo, shughuli mbalimbali zimefanyika ikiwemo dua na sala maalum za kuwaombea mashujaa waliotangulia mbele ya haki pamoja na kuliombea Taifa liendelee kuwa na amani na mshikamano.
#MillardAyoUPDATES Load More